Bei ya mafuta yashuka kwa 5% duniani


26 Mei 2017

Bei ya mafuta yashuka kwa 5% duniani

Waziri wa kawi nchini Saudia Khalid al-Falih
Waziri wa kawi nchini Saudia Khalid al-Falih

Bei ya mafuta imeshuka kwa asilimia 5 licha ya mataifa yanayozalisha bidhaa hiyo kukubaliana kupunguza kiwango cha uzalishaji kwa kipindi cha miezi minane.
Wakikutana mjini Vienna,mawaziri wa kawi kutoka muungano wa mataifa yanayozalisha mafuta OPEC na mataifa yasiozalisha bidhaa hiyo ulikubaliana kuendelea kupunguza kiwango cha mafuta hadi Machi 2018.
Lakini wawekezaji walikuwa na matumani kwamba wazalishaji hao wa mafuta wataendelea na mpango huo.
Mafuta ghafi yalishuka kwa dola 2.60 hadi dola 51.36 kwa pipa siku ya Alhamisi na yalikuwa yamefika dola 51.47 Ijumaa alfajiri.
Haki miliki ya pich
Waziri wa kawi nchini Saudia Khalid al-Falih aliyesimamia mkutano huo kama mwenyekiti mwenza na mwenzake wa Urusi Alexander Novak alisema: Tuliangazia vigezo kadhaa kutoka miezi 6, 9 na hadi 12 na pia tuliangazia uwezekano wa kupunguza uzalishaji huo kwa viwango vya juu.
Muungano wa mataifa ya OPEC na mataifa mengine 11 yasiozalisha mafuta ikiwemo Urusi, kwanza yalikubaliana kupugunza uzalishaji Disemba iliopita katika juhudi za kupiga jeki bei.
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: