Majaliwa akagua maandalizi sherehe za Muungano




Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amefanya ukaguzi wa miundombinu kwa ajili ya sherehe za miaka 53 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar na kusema kuwa maandalizi yake yako pazuri.
Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo leo mchana mara baada ya kupokea taarifa ya maandalizi na kukagua Uwanja wa Jamhuri ambapo sherehe hizo zitafanyika na uwanja wa Nyerere Square ambako zitafanyika burudani mbalimbali kama sehemu ya maadhimisho hayo.
“Nilikuja kuangalia maandalizi ya sherehe hizo yamefikia wapi, najua kutakuwa na maonyesho ya kijeshi zikiwemo michezo na burudani kutoka Tanzania Bara za Visiwani,” amesema.
Majaliwa alitumia fursa hiyo kuwakaribisha wakazi kutoka wilaya zote za Mkoa wa Dodoma na mikoa ya jirani wafike kwenye maadhimisho hayo ambayo kwa mara ya kwanza katika historia ya Tanzania yanafanyika mkoani humo.

Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: