MNH yaanza matibabu ya kuondoa uvimbe bila kupasua

 
THURSDAY, APRIL 6, 2017

MNH yaanza matibabu ya kuondoa uvimbe bila kupasua

 
Mafunzo hayo kwa madaktari wa Muhimbili
Mafunzo hayo kwa madaktari wa Muhimbili yanaendeshwa na Daktari aliyebobea katika upasuaji kwa njia ya matobo kutoka nchini Kenya Profesa Rafique Parkar .Picha na Herieth Makwetta 
By Haerieth Makwetta, Mwananchi hmakweta@mwananchi.co.tz
Dar es Salaam. Hospitali ya Taifa Muhimbili leo imeanza kufanya  matibabu ya kuondoa uvimbe 'fibroid' kwa wanawake bila kupasua ambao hufanyika kwa njia ya matundu madogo (laparoscopic Surgery).
Upasuaji huo uliofanyika leo katika chumba kikuu cha upasuaji, unaenda sambamba na mafunzo kwa vitendo kwa madaktari zaidi ya 30 ambao wanafuatilia moja kwa moja kwa njia ya luninga wakiwa chumba cha mkutano.
Akizungumza wakati wa upasuaji huo, Daktari Bingwa wa uzazi na magonjwa ya wanawake Vicent Tarimo alisema upasuaji wa aina hiyo kwa njia ya kawaida huchukua takribani saa moja na nusu mpaka mawili, lakini kwa njia hiyo ya kisasa wamefanikiwa kumtibu mwanamke aliyekuwa na uvimbe kwenye mirija ya uzazi kwa saa moja.
"Zaidi ya wanawake 15 watanufaika na upasuaji huu na wengi wamekuwa na tatizo la uvimbe sehemu mbalimbali kuzunguka kizazi," alisema.


 
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: