Papa Francis awasili nchini Misri


  • 28 Aprili 2017
Kiongozi wa kanisa katoliki duniani papa Francis awasili Misri kwa ziara ya kidini
Kiongozi wa kanisa katoliki duniani papa Francis awasili Misri kwa ziara ya kidini
Kiongozi wa kanisa katoliki duniani Papa Francis amewasili nchini Misri kwa ziara fupi inayolenga kuimarisha uhusiano wa kidini na ulimwengu wa Kiislamu.
Ziara hiyo inajiri wakati ambapo kuna ongezeko la mauaji ya Wakristo waliopo katika mashariki ya kati hususan wale wa jamii ya kanisa la Coptic.
Mapema mwezi huu kundi la Islamic state lilikiri kutekeleza shambulio la mabomu ya makanisa mawili ya Coptic.
Papa Francis atakutana na rais wa Misri na kutoa hotuba kuhusu amani katika chuo kikuu cha Al-Azhar, taasisi ya masomo ya Kiislamu miongoni mwa madheheu ya Sunni.
Ataonyesha umoja wake na mwenzake wa kanisa hilo Tawadrod II akijumuika naye katika kanisa lililoshambuliwa mnamo mwezi Disemba.
Uhusiano kati ya Vatican na Waislamu wengi ulishuka 2006 wakati mtangulizi wa Papa Francis Benedict alipoonekana akihusisha Uislamu na ghasia.
Kiongozi wa kanisa katoliki duniani papa Francis kuelekea Misri kwa ziara ya kidini
Image captionKiongozi wa kanisa katoliki duniani papa Francis awasili Misri kwa ziara ya kidini
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: