Ndege yatatiza urushaji wa roketi Marekani

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM

Shughuli ya kurusha roketi huko Virginia Marekani ilisimamishwa dakika za mwisho baada ya ndege ndogo kuruka karibu na eneo shughuli hiyo ilikuwa ifanyika.
Roketi hiyo ya mizigo isiyo na burani ilitarajiwa kurushwa kwenda kituo cha kimataifa kilicho anga za juu (ISS) wakati shughuli hiyo ilisitishwa ghafla.
Walikuwa wameona ndege ndogo iliyokuwa ikiruka eneo lisiloruhusiwa umbali ya futi 500 katika kisiwa cha Wallops.
Urushaji wa roketi hiyo utaradiwa tena leo Jumapili.
Roketi hiyo imesheheni kilo 3,356 ya chakula, vifaa na bidhaa za sayansi kwa kituo cha ISS
Orbital ATK, iliyo na kandarasi ya dola bilioni 1.9 na shirika la anga za juu la Marekani Nasa kupeleka bidhaa katika kituo cha ISS ilipeperusha matangazo ya urushaji wa roketi hiyo.

Tuma habari picha kwa 0625966236

Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: