Waziri mkuu Uhispania aapa kumaliza mzozo wa Catalonia

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM

Waziri mkuu wa Uhispania Mariano Rajoy amesema kuwa uchaguzi wa eneo la Catalonia mwezi ujao utasaidia kumaliza mzozo wa kijitenga katika eneo hilo la kaskazini mashariki mwa nchi.
Alihutubia mkutano wakati wa ziara yake ya kwanza tangu kutangaza udhibiti kamili eneo hilo.
Viongozi kadhaa waku wa Catalonia kwa sasa wanazuiliwa kufuatia hatua hiyo.
Takriban watu 75,000 waliandamana mjini Barcelona siku ya Jumamosi kupinga kukamatwa viongozi hao.
Hali hiyo ilichochewa na kura ya maoni iliyokumbw na utata ilyofanyika Catalonia mwezi Oktoba ambayo ilikuwa imezuiwa na mahakama za Uhispania.
Protesters shine their mobile phone torches in Barcelona, 11 NovemberHaki miliki ya pichaREUTERS
Image captionTakriban watu 75,000 waliandamana mjini Barcelona siku ya Jumamosi kupinga kukamatwa viongozi hao.
Maafisa huko Catalonia walisema kuwa kura hiyo ilipata asilimia 92 ya kura kutoka kwa watu asilimia 43 waliojitokeza.
Wengi wa wale waliopinga kura hiyo hawakupiga kura na walikataa kutambua uhalali ya kura hiyo.
Serikali ya Catalonia hatimaye ikatangaza uhuru. Kujibu hilo serikali ya Uhispania ilivunja bunge la Catalonia na katangaza udhibiti kamili na kuitisha uchaguzi wa mapema tarehe 21 Disemba.

Tuma habari picha WhatsApp 0625966236


Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: