Nyambizi ya Marekani yatia nanga Korea Kusini




 Meli  kubwa ya Kijeshi inayomilikiwa na jeshi la Marekani, imewasili na kutia nanga katika Pwani ya Korea Kusini.

Meli hiyo iitwayo, USS Michigan, imeongeza wasiwasi  kutokana na Marekani na Korea Kaskazini kujibizana vikali na kutoleana vitisho katika siku za karibuni.
Nyambizi ya USS Michigan hutumia nguvu za nyuklia na hubeba makombora aina  154 na wanajeshi 60 pamoja na meli nyambizi nyingine ndogo, gazeti la Korea Kusini la Chosun Ilbo limeripoti.
Meli hiyo inatarajiwa kushiriki kwenye mazoezi ya kijeshi pamoja na kundi la meli zinazoongozwa na Carl Vinson, kundi ambalo lilitumwa eneo la Korea kuonyesha ubabe wa kijeshi wa Marekani.




                                                 comment, like and share
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: