Operesheni ya Takukuru yaokoa Sh9bilioni

THURSDAY, APRIL 6, 2017

Operesheni ya Takukuru yaokoa Sh9bilioni

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akisoma hotuba ya
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akisoma hotuba ya bajeti ya ofisi ya Waziri Mkuu kwa mwaka wa fedha 2017/2018, mjini Dodoma leo .Picha na Edwin Mjwahuzi 
By Sharon Sauwa, Mwananchi mwananchipapers@mwananchi.co.tz
Dodoma. Serikali imeokoa Sh9.75 bilioni  katika mwaka  wa Fedha 2016/17 kutokana na operesheni zilizofanywa na Taasisi ya kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru).
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amesema hayo leo wakati akisoma bajeti ya Ofisi ya Waziri Mkuu na Bunge kwa Mwaka wa Fedha 2017/18 bungeni.
Amesema katika Mwaka wa fedha  2017/18 Serikali itaendelea na mapambano yake  dhidi ya rushwa hususan katika eneo la ukusanyaji wa mapato ya Serikali.
"Kudhibiti mqtumizi ya fedha  za umma na malipo hewa na kuimarisha ufuatiliaji na ukaguzi wa miradi ya maendeleo," amesema
Majaliwa amesema katika Mwaka wa Fedha 2016/17, Takukuru imefanya uchunguzi wa majalada 306 ya tuhuma za rushwa na kupata kibali cha Mkurugenzi wa Mashtaka nchini kuendelea na mashtaka kwa majalada 104.

 
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: