Polisi imewakamata watu wawili kwa biashara ya viungo vya binaadam


26 Mei 2017

Serikali ya Cambodia imepiga marufuku biashara ya viungo nchini Cambodia
Serikali ya Cambodia imepiga marufuku biashara ya viungo nchini Cambodia
Polisi nchini Cambodia imewakamata watu wawili wakishutumiwa kuwasafirisha watu takriban kumi kwenda nchini India kwa ajili ya kuchangia figo zao kwa ajili ya shughuli haramu ya kupandikiza viungo.
Watu hao, Mwanaume na mwanamke wanaoishi katika mji wa Phnom Penh wanaelezwa waliandaa safari hiyo kwa watu hao kwa ahadi ya malipo ya dola za kimarekani 6000 kila mmoja.
Raia wa Cambodia wenye uhitaji wa figo waliwalipa watu hao wawili dola 40,000 za Marekani kwa ajili ya Operesheni hiyo ya kupandikiza figo, nchini India.
Mwaka jana,Serikali ya Cambodia ilipiga marufuku biashara ya viungo, inayodaiwa kuwa haramu.
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: