Polisi Uingereza walalamikia kuvuja kwa picha za Manchester


25 Mei 2017

Picha za shambulio zilizochapishwa na gazeti hilo
Picha za shambulio zilizochapishwa na gazeti hilo
Polisi nchini Uingereza wameyalaumu machapisho yaliyotolewa katika gazeti la New York Times juu ya picha na taarifa kutoka katika eneo ambalo shambulio la bomu lilitokea mjini Manchester.
Maafisa nchini humo wanasema kuvuja kwa picha hizo kuna haribu uchunguzi wa polisi na kuondoa imani na washirika wao katika masuala ya kiintelejinsia.
Picha hizo zinaonesha vitu mbalimbali ambavyo vingetumika kama ushahidi kama vile betri na vitu vingine vyenye muonekano wa vilipuzi.
Hata hivyo gazeti hilo la Marekani limejitetea juu ya picha hizo ambazo imesema zinaashiria kuwa bomu lililotumika katika shambulio hilo kwa kiasi kikubwa linaonekana kuwa ni la kisasa.
Waziri mkuu wa Uingereza anatarajiwa kulipeleka suala hilo kwa Rais wa Marekani Donald Trump wakati wa mkutano wa nchi wanachama wa Jumuia ya NATO, ambao unafanyika leo.
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: