Makaburi yaliyo na 'ujumbe kutoka kuzimu' yagunduliwa Misri

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM=>

Egyptian antiquities worker is seen inside the recently discovered burial site in Minya, Egypt
Makaburi ya zamani ambayo yana majeneza kadha yaliyotengenezwa kwa mawe, na mkufu ulio na "ujumbe kutoka kuzimuni" vimegunduliwa nchini Misri.
Ugunduzi huo umefanywa Minya, kusini mwa Cairo. Makaburi yaliyogunduliwa ni ya zaidi ya miaka 2,000 iliyopita na shughuli ya ufukuzi inatarajiwa kuchukua miaka takriban mitano.









LHaki miliki ya pichaREUTE

Waziri wa mambo ya kale Misri Khaled al-Enany amesema makaburi hayo yana majeneza 40, vito, vyungu na barakoa ya dhahabu.
Amesema kuna mashimo ya kuwekwa majeneza chini ya ardhi ambayo ni ya enzi za Mafirauni hadi enzi za Wagiriki mnamo mwaka 300BC hivi.
"Huu ni mwanzo tu wa ugunduzi huu mpya," aliwaambia waandishi wa habari.
"Karibuni tutaanza kuongeza kivutio kingine cha mambo ya kale Misri."

Ancient statues discovered near an ancient necropolis in Minya, EgyptHaki miliki ya pichaREUTERS

Mostafa Waziri, mkuu wa ufukuzi huo, amesema makaburi manane yaligunduliwa katika kipindi cha miezi mitatu iliyopita lakini anatarajia mengine zaidi yagunduliwe.
"Shughuli ya ufukuzi inapangiwa kuendelea kwa miaka mitano hivi katika jaribio la kufukua eneo lote la makaburi," amesema.

Presentational grey line

Bw Waziri amesema mengi ya makaburi na vitu vya kale vilivyogunduliwa ni vya makasisi wa miungu wa zamani wa Misri kwa jina Thoth.

An Egyptian archaeologist works on a sarcophagus at the site of an ancient Egyptian cemetery that was uncovered, in Minya province, 245 km south of Cairo, EgyptHaki miliki ya pichaEPA

Magudulia manne yenye vifuniko ambayo yamehifadhiwa vyema yameundwa kuwa na muonekano wa wana wanne wa kiume wa miungu Horus pia yaligunduliwa.
"Bado magudulia hayo yana viungo vya ndani ya mwili vya marehemu vilivyohifadhiwa vyema ndani. Magudulia hayo yamepambwa kwa maandishi ya kale yanayoonesha majina na vyeo vya wahusika," amesema Bw Waziri.
Ameeleza sifa ya kugunduliwa kwa mkufu huo Mkesha wa Mwaka Mpya ukiwa umeandikwa ujumbe "kheri ya mwaka mpya" ni ya ajabu.
"Huu ni ujumbe uliotumwa kwetu kutoka kuzimuni," amesema.

Four canopic jars, made of alabaster with lids bearing the faces of the four sons of god Horus, that were unearthed are displayed at the site of an ancient Egyptian cemetery, in Minya province, 245 km south of Cairo, Egypt.Haki miliki ya pichaEPA

Mapema mwezi huu, wanaakiolojia waligundua kaburi la kasisi wa kike ambaye alizikwa miaka 4,400 iliyopita.
Kaburi hilo lilikuwa limehifadhiwa vyema na lilikuwa na picha ya ukutani ya kasisi huyo, Hetpet, zikimuonesha akitekeleza shughuli mbalimbali.
Kwa Injili Bofya hapa
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: