Mhubiri wa injili Billy Graham, afariki dunia akiwa na umri wa miaka 99

Mhubiri wa injili Billy Graham, aliyepata umaarufu mkubwa duniani katika karne ya 20 amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 99.
Graham, raia wa Marekani, alieanzia kuhubiri jijini London Uingereza mnamo mwaka 1954, alikusanya maelfu ya watu kila mahali alipofanya mikutano ya hadhara ya injili.
Afrika Mashariki, Graham aliwahi kuhubiri Tanzania, miaka 55 iliyopita, wakati nchi iliitwa Tanganyika, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya Afrika miaka ya 1960. Takriban "watu 40,000 walihudhuria mkutano huo wa siku moja, tarehe Feb 28. 1960", kwa mujibu wa mtandao wa shirika lake.
Pichani, akiwa katika ziara ya uinjilisti Arusha, Tanganyika mwaka 1960.
Kwa zaidi ya miaka 60 inakadiriwa kuwa amehubiri kwa jumla ya watu milioni 210.
Alikuwa Mkristo akiwa na umri wa miaka 16 baada ya kumsikiliza mhubiri mmoja na kuanza huduma ya mahubiri mwaka 1939.


By the time this graduation picture was taken he had found his callingHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionWakati akifuzu Billy tayari alikuwa amepata wito wa injili

Graham, ambaye alifanya kazi kama afisa wa mauzo, aliendelea na kuwa mmoja wa wahubiri wenye ushawishi mkubwa miongoni mwa watu wa dini zote huku akiwashauri marais na viongozi wengine wengi duniani juu ya imani ya Kikristo.
Mwaka 1949, alipata umaarufu wakati alihubiri kwa wiki nane kwenye hema kubwa huko Los Angeles.
Wakati wa harakati za mashirika ya kupigania haki za binadamu, Graham aliibuka kuwa mkasoaji mkubwa wa ubaguzi wa rangi nchini Marekani.


Graham (l) in the Canvas Cathedral with his music director Cliff BarrowsHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionGraham(kulia) akiwa ni msimamizi wake wa muziki Cliff Barrows

Ni muhubiri aliyeepuka kashfa mbalimbali zilizowazonga wahubiri wengi waliotumia runinga kusambaza injili.
Alijenga uhusiano wa kirafiki na marais kadhaa wa Marekani kuanziaTruman hadi Nixon na hata Obama. Mkutano wake wa mwisho wa hadhara ulikuwa mwaka 2005 jijini New York Marekani akiwa na umri wa miaka 86.
Rais Donald Trump amemuelezea Graham kama "mwanaume wa kipekee".
Akiandika kwenye ukurasa wake wa Twitter, Trump amesema "Mhubiri maarufu wa Injili Billy Graham. Hakuna aliyekuwa kama yeye! Atakumbukwa na Wakristo na watu wa dini zote. Mwanamume wa kipekee kabisa."


Thousands flocked to hear him preach in London in 1954Haki miliki ya pichaGETTY IMAGES
Image captionMaelfu walifika kusikiza akihubiri London mwaka 1954
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: