Donald Trump: Nitaleta amani kati ya Israel na Palestina


  • 4 Mei 2017
Rais Donald Trump ameapa kutataua mzozo wa mashariki ya kati
Rais Donald Trump ameapa kutataua mzozo wa mashariki ya kati
Rais wa Marekani Donald Trump amesema kuwa kuna uwezekano mkubwa kupatikana kwa amani mashariki ya kati katika mazungumzo na rais wa Palestina Mahmoud Abbas.
Katika taarifa ya pamoja waliotoa kwa vyombo vya habari rais Trump aliapa kwamba ''tutahakikisha hili linatendeka''.
Bwana Abbas alimuambia Trump katika ikulu ya Whitehouse kwamba anataka kuwepo kwa makubaliano ya amani ya mpango wa kudumu wa mataifa mawili yalio huru ikiwemo mipaka iliokuwepo kabla ya 1967.
''Sasa rais tuna matumaini na wewe'',alisema bwana Abbas.
Hatahivyo bwana Trump amekuwa na mawazo tofauti kuhusiana na utatuzi wa mataifa mawili yalio huru.
Rais wa Palestina Mahmoud Abbas
Image captionRais wa Palestina Mahmoud Abbas
Mnamo mwezi Februari alisema kuwa anachukulia swala la taifa moja na mataifa mawili yalio huru na napenda wazo ambalo linaungwa mkono na mataifa yote mawili.
Siku ya Jumatano, rais huyo wa Marekani alisistiza kwamba hakutakuwa na amani ya kudumu hadi mataifa yote mawili yatakapopata njia ya kusitisha uchochezi wa ghasia.
Kiongozi huyo wa Palestina anashinikizwa kusitisha malipo kwa familia za wafungwa wa Kipalestina pamoja na zile za wale waliouawa katika mzozo dhidi ya Israel.
Serikali ya Israel inasema kuwa malipo hayo yanachochea ugaidi, lakini maafisa wa Palestina wanasema kuwa kusitisha malipo hayo itakuwa pigo la kisiasa kwa rais Abbas ambaye hana umaarufu mkubwa nyumbani.
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: