Mwanamke mzito duniani kufanyiwa matibabu ya viungo


5 Mei 2017
Eman Abd El Aty
Mwanamke raia wa Misri aliyetambulika kuwa mtu mzito zaidi duniani amelazwa katika hospitali moja mjini Abu Dhabi ili kuendelea na matibabu.
Eman Abd El Aty anayedaiwa kuwa na kilo 500 aliondoka hospitali ya India siku ya Alhamisi baada ya madaktari kusema kuwa amepoteza takriban kilo 250.
Alisafirishwa kupitia ndege ya abiria hadi UAE
Madaktari wanasema kwamba atafanyiwa matibabu ya viungo.
Katika majuma ya hivi karibuni kulizuka ugomvi kati ya madaktari wake India na familia yake.
Madaktari wakimsaidia bi Eman akuingia katika ambalensi ili kusafirishwa hadi Abu Dhabi kwa matibabu zaidi
Image captionMadaktari wakimsaidia bi Eman akuingia katika ambalensi ili kusafirishwa hadi Abu Dhabi kwa matibabu zaidi
Ugomvi huo ulianza baada ya dadake Shaimaa Selim kutoa kanda ya video katika mtandao wa kijamii kwamba dadaake alikuwa bado hawezi kuzungumza ama hata kutembea na kwamba hakupoteza kilo nyungi kama ilivyoarifiwa na hospitali hiyo.
Hospitali hiyo ilikana madai hayo.
Bi Selim alitaka dadake kusalia katika hospitali hiyo hadi atakapoanza kutembea, lakini madaktari wa mifupa katika hospitali hiyo walisema kuwa hatotembea tena.
Madaktari na wauguzi waliandamana na mwanamke huyo hadi Abu Dhabi kulingana na ripoti.
Upasuaji wa utumbo ulivyofanyika
Image captionUpasuaji wa utumbo ulivyofanyika
Alikuwa amewasili nchini India kwa kutumia ndege ya kubeba mizigo mnamo mwezi Februari na akawa akiwekwa maji pekee ili kupunguza uzani wake ili madaktari waweze kumfanyia upasuaji wa kupunguza tumbo lake.
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: