Tucta yawazungumzia walioghushi vyeti serikalini


 1 Mei 2017

Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya
Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta), Dk Yahya Msigwa  

Katibu Mkuu wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (Tucta), Dk Yahya Msigwa amesema wafanyakazi wa umma 9,932 waliobainika kuwa na vyeti bandia wakiacha kazi kwa hiari watakuwa wamekosa viinua mgongo vya miaka waliyoitumikia Serikali.
Ijumaa iliyopita, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Utumishi na Utawala Bora), Angellah Kairuki alimkabidhi Rais John Magufuli ripoti ya majina hayo ambayo yameibua mjadala mitaani na mitandaoni.
Akizungumzia suala hilo, Dk Msigwa amesema kama watumishi hao wataendelea kubaki kazini watashtakiwa kwa kughushi vyeti na kujipatia mshahara kinyume na sheria.
“Hapa kuna mtego wahusika wenyewe wataamua kama waendelee na kazi ili waje washtakiwe au kujiondoa mapema na kuacha kiinua mgongo chao,” amesema katibu huyo.
Kwa mujibu wa Sheria ya Kazi na Uhusiano Kazini namba 6 ya mwaka 2004, mwajiri anawajibika kumlipa haki zake mfanyakazi pale anapomwachisha kazi.
Hata hivyo, Dk Msigwa amesema Serikali ikiamua kuwafukuza kazi kwa sheria hiyo ni lazima walipwe stahiki zao kwa sababu wameondolewa kwenye ajira kwa lazima.
“Kwa sheria ya kazi namba sita (ya mwaka 2004) hakuna neno kufukuzwa kazi, ukimwondoa kazini mtumishi ni lazima umlipe kiinua mgongo, ndiyo maana hapa ninaona agizo la Rais Magufuli ni mtego ili waache kazi wenyewe,” alisema.
Baada ya kupokea ripoti hiyo, Rais Magufuli aliwataka wafanyakazi hao kuacha kazi ndani ya siku 15 vinginevyo wakumbane na mkono wa sheria baada ya kuviagiza vyombo vya ulinzi na usalama kuwachukulia hatua.
 Mshirikishe Mwenzako: zakacheka.blogspot.com/ www.zakacheka.simplesite.com +255 625966236
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: