Vurugu na maandamano yatanda siku ya Mei Mosi;Venezuela

  • 2 Mei 2017

Venezuela
Rais wa Venezuela, Nicolas Maduro, ametoa wito wa kuundwa kwa kwa Bunge la katiba

                                                                                                                                                        Siku ya wafanyakazi duniani haikua na mwisho mwema nchini Venezuela baada ya kutokea vurugu na maandamano mara baada ya rais wa Venezuela Nicolas Maduro kuhutubia taifa akitangaza kuundwa kwa Bunge jipya ili kumaliza mgogoro wa kisiasa nchini humo.
Rais Maduro, alitoa wito wa kuundwa kwa kwa Bunge la katiba ambalo litakuwa na mamlaka ya kuandika katiba mpya,kwa madai kuwa chombo hicho kipya kitaundwa na raia wa kawaida,na kuachana na bunge la kitaifa linalodhibitiwa na upinzani
Hata hivyo kiongozi wa Upinzani, nchini humo, Henrique Capriles amesema chombo hicho kipya kitakuwa kina malengo ya kuhujumu katiba .

Venezuela
Image captionwanaharakati kutoka upande wa upinzani

Bunge la kitaifa limekuwa likitaka Rais Maduro ajiuzulu wakati taifa hilo likikabiliwa na hali mbaya ya kiuchumi.
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: