Watu 12 wauwawa katika shambulio la kwanza la 'IS' nchini Iran


8 Juni 2017

Picha hii ya kituo cha Far News inaonyeha mlipuko nje ya kaburi
Picha hii ya kituo cha Far News inaonyeha mlipuko nje ya kaburi

Wanajeshi wa Iran wananyatia huku wakizingira majengo ya Bunge
Wanajeshi wa Iran wananyatia huku wakizingira majengo ya Bunge

Picha hii inaonesha mtoto akishushwa dirishani kutoka kwenye majengo ya Bunge
Picha hii inaonesha mtoto akishushwa dirishani kutoka kwenye majengo ya Bunge

Shrine of the late Ayatollah Ruhollah Khomeini at Khomeini's mausoleum in Tehran (2009)
Kaburi la Ayatollah Khomeini kusini mwa Tehran


Mashambulio mawili ya kujitoa mhanga katika Bunge la Iran na kwenye eneo la kaburi la kiongozi wa kidini Ayatollah Khomeini kwenye mji mkuu wa Iran, Tehran, yamesababisha vifo vya watu 12 na wengine wengi kujeruhiwa.
Mashambulio hayo katika jumba la Bunge, kwa sasa inaonekana imemalizika, baada ya masaa kadhaa ya kuzingirwa, huku milio ya risasi ikisikika.
Mlipuaji mmoja wa kujitoa kufa aliyekuwa amevalia vilipuzi, alijilipua katika eneo hilo la kumbukumbu na kaburi la Khomeini.
Maafisa wa usalama wa Iran wamefaulu kuzima shambulio hilo.
Haki miliki ya pi
Mashambulio hayo yalifanyika vipi?
Watu waliokuwa wamejihami na bunduki aina ya AK, waliingia ndani ya majengo ya Bunge, Jumatano asubuhi.
Picha kutoka mahala pa tukio zilionyesha operesheni kali ya walinda usalama, huku wanajeshi wakizingira bunge.
Milio mikali ya risasi zilisikika.
Haki miliki 
Kundi la Islamic State (IS), limekiri kutekeleza mashambulio hayo, ambayo ni ya kwanza kutokea nchini Iran.
IS imeweka picha mtandaoni, inayodai kuwa ni ndani ya majengo ya Bunge.
Duru zinasema kwamba washambuliaji hao wenye silaha waliingia Bungeni kupitia lango la raia, wakivalia kama wanawake.
Runinga ya taifa ya Iran baadaye iliripoti kuwa, washambuliaji wanne walioingia ndani ya majengo ya Bunge, wameuwawa na walinda usalama.
Mamlaka kuu nchini Iran inapinga dhana kuwa, kunao watu waliozuiliwa matenga ndani ya majengo hayo ya Bunge.
Shirika la habari la Iran IRIB lilimnukuu mbunge mmoja akisema kuwa kulikuwa na washambualiaji kadha ndani ya majengo ya bunge waliokuwa wamejihami na bunduki aina ya AK-47.
Shirika hilo la habari lilisema kuwa walinzi wawili walijeruhiwa.
Ripoti zinasema kuwa ufyatuaji risasi katika kaburi la Ayatollah Khomeini ulifanyika wakati mmoja.
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: