Mlipuko Kagera Tanzania waua wanafunzi sita

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM
Baadhi ya wajeruhi wakipata matibabu katika hosipitali ya Rulenge, Ngara
Badhi ya wajeruhi wakipata matibabu katika hosipitali ya Rulenge, Ngara
a
Wanafunzi sita wa shule ya msingi Kihinga mkoani Kagera kaskazini magharibi mwa Tanzania wamefariki dunia na wengine 41 wamejeruhiwa baada ya kulipukiwa na bomu wakicheza.
Kamanda wa polisi wa mkoa, Augustine Oromi huo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na tayari wananchi wamejitokeza kuchangia damu kwa ajili ya kuwasaidia majeruhi.
Mkoa wa Kagera ni eneo linalowahifadhi wakimbizi kutoka nchi jirani kama Burundi. Baadhi ya wakimbizi hao walikuwa wanajeshi ambao waliacha silaha zao katika baadhi ya makambi.
Kamanda wa polisi wa mkoa, Augustine Oromi amesema tayari timu ya upelelezi imetumwa katika eneo hilo kuchunguza sehemu ambapo bomu lililipukia.
Watoto wakipata huduma katika hosipitali ya Rulenge baada ya mlipukoHaki miliki ya picha
Watoto wakipata huduma katika hosipitali ya Rulenge baada ya mlipuko
Kwa mujibu wa Dokta Mariagoreth Fredrick ambaye ni mganga mkuu hosipitali ya Rulenge, amethibitisha kupokea miili hiyo na majeruhi ambao baadhi wako katika hali mbaya na tayari wanapatiwa matibabu.
"Tulionao hali ya sio nzuri. Wengine wameumia matumbo, wengine wamechanika bandama, wengine wamevunjika miguu, wengine vichwa vimepata majeraha, wengine wameumia macho." Dokta Mariagoreth ameiambia BBC.
Inaelezwa kwamba kabla ya kulipukiwa na kifaa hicho kinachoarifiwa kuwa ni bomu, wanafunzi hao walikuwa wanakichezea.

TUMA HABARI, PICHA WhatsApp kwa 0625966236

Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: