Bandari ya nchi kavu kujengwa Arusha





Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo
Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo amesema Serikali ina mpango wa kujenga bandari ya nchi  kavu mkoani hapa.
Akizungumza  katika Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Meru, Gambo amesema  bandari hiyo itajengwa ili kurahisisha usafirishaji wa mizigo hususan malighafi za viwanda na bidhaa jambo ambalo litachochea uchumi wa mkoa huo na Taifa kwa ujumla.
Gambo amesema zaidi ya ekari 500 zitatengwa kwa ajili ya kusaidia kufanikisha mchakato huo.
“Jamani kujengwa kwa bandari hiyo kutasaidia sana kurahisisha maendeleo katika wilaya hii na mkoa wetu ,hivyo tunaomba wananchi wa Arusha mtoe ushirikiano katika kufanikisha suala hili,”

Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: