Bulaya alalamikia wapinzani wanavyoumia bungeni




Mbunge wa Bunda Mjini (Chadema), Ester Bulaya amesema hata kama wamekuwa wakinyamaza, haina maana kwamba wapinzani hawaumizwi na mambo wanayofanyiwa bungeni.
Bulaya alisema hayo jana wakati akichangia hotuba ya bajeti ya Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo bungeni mjini Dodoma.
“Tukitoka mnasema, tukikaa mnatunyanyasa. Mnataka tufanye nini? Leo mko madarakani, kesho hamko madarakani. Kwa nini mnatuchagulia cha kusema?” alihoji Bulaya.
Mbunge huyo alitoa kauli hiyo kufuatia Mwenyekiti wa Bunge, Azzan Zungu kuzuia baadhi ya maneno yaliyomhusisha aliyekuwa msaidizi wa mwenyekiti wa Chadema, Ben Saanane kuagiza yafutwe katika kitabu cha hotuba ya upinzani.
Saanane alipotea katika mazingira ya kutatanisha na hadi sasa suala la mahali alipo halijawahi kuwa wazi, hivyo kuibua sintofahamu nchini.
Baada ya kauli hizo, Zungu ambaye jana alionekana dhahiri kumvumilia msemaji wa upinzani wa wizara hiyo,
Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ alisema, “kiti hiki hakiongozwi na Serikali na hakina mrengo wa Serikali. Nimeshatoa ruling na ruling zangu hazihojiwi humu, bali kwa kufuata kanuni ya tano. Unaandika barua kwa katibu wa Bunge naye anaiwasilisha kwa Spika.”
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: