Kijana adaiwa kujiua kwa sababu ya mchezo mtandaoni Kenya


9 Mei 2017

Visa vya watu kujitoa uhai kutokana na michezo ya mtandaoni havijathitishwa

Polisi nchini Kenya wanafanya uchunguzi kubaini iwapo kijana mmoja alijiua baada ya kushiriki mchezo wa mtandaoni, vyombo vya habari nchini humo vimeripoti.
Mkuu wa polisi wa Nairobi Japheth Koome amesema wanachunguza taarifa kwamba kijana wa miaka 16 alijitoa uhai kutokana na mchezo huo.
Kituo cha Centre for Safe Internet cha Bulgaria kinasema kufikia sasa hakuna ushahidi wa kutosha kuthibitisha vifo vilivyotokana na kucheza mchezo huo.
Mchezo huo unadaiwa kuwapa changamoto washriiki wafanya mambo ya kutisha, ambapo jambo la mwisho linakuwa ni kujitoa uhai.
Taarifa kuhusu mchezo huo vimeripotiwa nchini Brazil na Urusi lakini hakuna visa vyovyote vya watu kujitoa uhai ambavyo vimethibitishwa rasmi kwamba vilitokana na mchezo huo kufikia sasa.
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: