Macron adai kampeni yake imedukuliwa Ufaransa


6 Mei 2017

Mgombea wa urais nchini Ufaransa Emmanuel Macron amedai kwamba wadukuzi waliidukua kampeni yake
Kamati ya kampeni ya mmoja wa mgombea wa urais nchini Ufaransa, Emmanuel Macron, imesema kuwa imevamiwa vikali na makundi ya udukuzi ambayo yamechapisha habari muhimu ya kundi lao katika mitandao ya kijamii.
Washiriki wa Bwana Macron wamesema kuwa barua pepe sahihi zimeibwa katika tarakilishi zao na kuchanganywa na zile bandia ili kuonyesha kuwa kamati hiyo ya Bwana Macron ni ya ubabaishaji tu.
Mpinzani mkuu wa Macron katika uchaguzi wa Urais nchini Ufaransa Marine Le Pen
Image captionMpinzani mkuu wa Macron katika uchaguzi wa Urais nchini Ufaransa Marine Le Pen
Chama cha Bwana Macron kijulikanacho nchini kama "En Marche" kilisema kuwa wachapishaji wa habari hizo zilizovurugwa wana nia ya kuvuruga demokrasia kabla ya uchaguzi wa marudio ya hapo kesho.
Tume ya Uchaguzi nchini Ufaransa inatarajiwa kuongoza mkutano wa dharura baadaye hii leo kujadili madai hayo ya udukuzi.
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: