Republicans watilia 'shaka' muswada wa afya wa Trump


 6 Mei 2017


Kiongozi wa chama cha Democrats bungeni Nancy Pelosi
Seneta maarufu katika chama cha Rais Trump cha Republican ameonya kuwa haitakuwa rahisi kwa wabunge kukubaliana juu ya mpango mpya wa kuchukua nafasi ya bima ya afya iliyoanzishwa na Rais Mstaafu Barack Obama ijulikanayo kama Obamacare.
Obamacare ulikuwa mfumo wa bei nafuu wa bima ya afya.
Lakini Seneta mwingine, Orinn Hatch atakayeshiriki katika kutunga sheria mpya ya kufutiliwa mbali mfumo wa bima ya Obamacare alisema licha ya upinzani mkali atahakikisha wabunge wanapitisha hoja hiyo.
Mnamo Alhamizi bunge la wawakilishi lilipitisha kwa uchache wa kura sheria inayokusudia kufutilia mbali mfumo wa bima wa Obamacare.
Rais wa Marekani Donald Trump amebuni muswada mpya wa afya utakaouondoa ule wa Obamacare
Image captionRais wa Marekani Donald Trump
Hata hivyo wanachama wa Republican wana wabunge wachache tu kuwazidi wenzao wa Democratic na kuna baadhi ya hao Warepublican ambao hawaungi mkono kufutiliwa mbali kwa mfumo wa bima ya Obamacare.
Naye Seneta wa chama cha Democratic, Bernie Sanders amesisitiza kuwa muswada huo wa bima wa chama cha Democratic hautapitishwa kwenye bunge la Seneti, akisema mswada huo unapaswa kutupwa chooni wala sio kupitishwa na ye yote.
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: