Vita vyaathiri usambazaji wa misaada CAR



UN imesema kuwa mashirika ya kutoa misaada ya kimataifa yamepunguza shughuli zake katika Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR


                                                                 6 Mei 2017
Umoja wa Mataifa umesema kuwa mashirika ya kutoa misaada ya kimataifa yamepunguza shughuli zake katika Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR kufuatia mashambulizi kadhaa dhidi ya wafanyakazi wao.

Mashirika manne ya kimataifa yamesitisha shughuli zake katika eneo la Ouham na Madkatari wasio na mipaka MSF wamesema kuwa wanawatibu wagonjwa wanaohitaji huduma za dharura pekee.
Umoja wa Mataifa unakisia kuwa nusu ya raia wote wa CAR hutegemea chakula na madawa ya misaada kila siku.
Taifa hilo limevurugika kutokana na mapigano kati ya makundi mawili ambayo asili yake ni kundi la zamani la Kiislamu la Seleka, lililompindua Rais mwaka 2013.
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: