Chama cha Macron chapata ushindi wa viti vingi bungeni



19 Juni 2017

Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron
Chama kinachoongozwa na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron kimeibuka na ushindi wa viti vingi katika bunge la nchi hiyo, wiki kadhaa baada ya ushindi wake wa nafasi hiyo ya Urais.
Zikiwa karibu kura zote zimehesabiwa chama chake cha Republique en Merche, sambamba na washirika wao MoDem, walipata zaidi ya viti 300 kati ya viti 577 vya bunge la nchi hiyo.
Akilihutubia taifa Waziri mkuu wa Ufaransa, Edouard Phillippe, amesema amezielezea kura hizo zilizopigwa kuwa ni za matumaini.
Chama hicho kinachoongozwa na Rais Macron kiliundwa tu mwaka uliopita na nusu ya wagombea wake wana udhoefu mdogo wa masuala ya kisiasa huku wengine wakiwa hawana kabisa.
Matokeo hayo ya kura yamempa nguvu na uwezo Rais huyo mwenye umri wa miaka 39 wa kuwa na mamlaka ndani ya bunge la nchi hiyo na kuweza kuendelea na msimamo wake wa kufanya mabadiliko aliyoyanadi katika kampeni zake za uchaguzi.
Lakini hata hivyo, wapiga kura wachache walijitokeza katika awamu hiyo ya pili ya uchaguzi wa Bunge, kushinda ilivyo tarajiwa, huku rekodi yake ikikadiriwa kushuka kwa karibu asilimia 42, kulinganisha na miaka mitano iliyopita.
Katika uchaguzi huo, kiuongozi wa chama cha mrengo wa kulia Marine Le Pen, alipata ushindi kwa mara ya kwanza.
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: