Rais Magufuli ateua mwenyekiti wa bodi TIC


15 Juni 2017


Rais John Magufuli amemteua Profesa Longinus Rutasitara kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC).
Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa jana (Jumatano) na Profesa Adolf Mkenda, Katibu Mkuu, Biashara na Uwekezaji, imesema uteuzi huo umeanza Mei 31.
Baada ya uteuzi huo, Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji, Charles Mwijage amewateua wajumbe sita wa bodi hiyo.
Wateule hao ambao uteuzi wao umeanza Mei 31 ni Profesa Winester Anderson, Dk Khatib Kazungu, Godfrey Simbeye, Dk Tausi Kida, Seif A. Seif na Mhandisi Peter Chisawilo.
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: