Rais Paul Kagame kuapishwa Rwanda

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM

18 Agosti 2017

Zachary B. John 0625 96626

Rais Paul Kagame wa Rwanda
Rais Paul Kagame wa Rwanda


Rais wa Rwanda Paul Kagame anaapishwa leo kuiongoza nchi hiyo kwa muhula wa tatu wa miaka 7.
Hii ni baada ya kushinda uchaguzi wiki mbili zilizopita kwa kupata asilimia 98 ya kura.
Sherehe za kula kiapo zinafanyika kwenye uwanja wa taifa Amahoro mjini Kigali.
zaidi ya marais 20 kutoka mataifa ya Afrika wanahudhuria sherehe hizo.
Miongoni mwao ni rais wa Sudan Omar Al Bashir ambaye anasakwa na mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita ICC.
Rwanda siyo mwanachama wa mahakama hiyo.
Katika uchaguzi wagombeaji wengine 2 Philippe Mpayimana na Frank Habineza wa chama cha Green waliambulia asilimia 1 jumla ya kura zao.
Uchaguzi huo ulikosolewa na baadhi ya mataifa kama Marekani ambayo ilisema hali ya siasa nchini Rwanda inatoa fursa tu kwa mtu mmoja pekee kwendelea kuiongoza nchi hiyo.
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: