Mwanasiasa wa upinzani ahukumiwa kifungo cha miaka 25 jela Cameroon

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM
31 OKTOBA 2017
Rais Paul Biya ameliongoza taifa hilo kwa miongo mitatu
Shirika la haki za binadamu la Amnesty International limeikosoa mahakama ya kijeshi nchini Cameroon kwa kumhukumu kiongozi mmoja wa upinzani miaka 25 jela kwa makosa ya kuchochea uasi.
Aboubakar Siddiki - kiongozi wa chama cha upinzani kaskazini mwa nchi, ndiye mwanasiasa aliyepelekwa jela katika harakati za Cameroon za kuuzima upinzani hivi karibuni.
Hakuna ushahidi uliotolewa mahakamani kuchangia hukumu kama hiyo , taarifa ya Amnesty International ilisema.
Alikamatwa mwaka 2014 baada ya kulaumiwa kwa kupanga kuipindua serikali ya Rais Paul Biya.
Bwana Biya amekuwa madarakani tangu mwaka 1982 na wakosoaji wake wanamtaja kuwa dikteta.
Watu kadhaa wameuawa na mamia kukamatwa wakati wa maandamano katika eneo hilo lenye watu wanaozungumza lugha ya Kiingereza na ambao wanalalamika kutengwa.
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER Zakacheka News Line

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: