Catalonia kufanya uchaguzi wake mkuu leo

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM=>
Raia wa Catalonia leo hii watachagua viongozi wao wapya, katika uchaguzi ambao serikali kuu ya Uhispania inaamini utamaliza msuguano wa kisiasa unaoendelea.
               Tangazo

Serikali kuu ya Madrid iliuvunja utawala uliokuwepo awali, baada ya kuandaa kura ya maoni iliyotajwa kuwa haikufuata kanuni, iliyotaka uhuru wa eneo hilo.
Watu wengi wanatarajiwa kushiriki katika uchaguzi huu
Image captionWatu wengi wanatarajiwa kushiriki katika uchaguzi huu
Rais wa Catalonia aliyeondolewa madarakani, Carles Puigdemont, amekuwa akiendeleza kampeni zake za kujitenga na Madrid akiwa uhamishoni chini Ubelgiji kwa kupitia mitandao ya kijamii.
Mwezi Oktoba yalifanyika maandamano makubwa ya Catalonia kutaka kujitenga na Hispania
Image captionMwezi Oktoba yalifanyika maandamano makubwa ya Catalonia kutaka kujitenga na Hispania
Takwimu zinaonyesha kuwa vyama vinavyotaka kujitenga na vile vinavyotaka kusalia kwenye serikali ya Madrid vinalingana katika kura za maoni.
Kuna kila dalili uchaguzi huu ukaibua tena hisia za kutaka kujitenga kuliko kutatua matatizo.
• Tuma habari picha na video za matukio mbalimbali WhatsApp kwa 0625966236
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: