Kamanda wa kikosi cha ulinzi wa rais I. Coast afungwa miaka 18 jela


 
Brunot Dogbo Ble
Aliyekua kamanda wa kikosi cha ulinzi wa Rais{ Republican Guards}, nchini Ivory Coast amehukumiwa miaka 18 gerezani kutokana na mauaji ya mwaka 2011 mjini Abdijan.
Brunot Dogbo Ble na wengine tisa walipatikana na hatia ya utekaji nyara na mauaji ya wanaume wanne wakiwemo raia wawili wa Ufaransa katika hoteli moja.
Utekaji nyara huo ulifanyika wiki za mwisho za vita vya wenyewe kwa wenyewe ambavyo vilizuka baada ya Laurent Gbagbo kung'angania madaraka licha ya kushindwa katika uchaguzi wa Urais mwaka wa 2010.
Aliyekua mkuu wa Polisi wakati huo Osee Longuey alihukumiwa miaka 20 jela.
Wanajeshi wengine wanne wa zamani walipata hukumu ya chini.
Kuna wengine ambao walipatikana bila makosa.
Taarifa zinasema mkuu huyo wa kikosi cha Ulinzi wa Rais aliwateka waathiriwa wake na kuwapeleka katika ikulu ya Rais ambapo waliteswa na kuuawa.
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: