Putin na Macron kutafuta suluhu ya kisiasa


29 Mei 2017

France
Rais Vladimir Putin na Emmanuel Macron
Rais wa ufaransa Emmanuel Macron amemwambia mshirika wake wa Urusi Vladimir Putin kuwa kipaumbele chao kinapaswa kuwa ni kutafuta suluhu ya kisisasa huko Syria ili kuondokana na vitisho vya kigaidi. Katika mkutano wao uliofanyika katika ikulu ya Versailles karibu na mji wa Paris, wawili hao walikubaliana kurudisha mazungumzo na Ujerumani juu ya Ukraine.
Rais Putin ameomba kuondolewa vikwazo kwa Urusi , akisema kuwa havisaidii chochote.
Vilevile rais Putin amekataa kuhusika kwa Urusi katika uchaguzi wa Ufaransa uliomalizika hivi karibuni, amesema kuwa kukutana kwake na mshindani wa Macron Bi Marine Le Pen hakukuwa na uhusiano wowote na matokeo ya Uchaguzi.
Macron alijaribu kutoa ufafanuzi wa maamuzi yake ya kufungia vyombo viwili vya Habari kutoka urusi akidai kuwa vinasambaa habari za uongo kuhusu yeye kipindi cha Kampeni.

Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: