Ujenzi wa hospitali ya mama na mtoto waanza Mirerani



 Kampuni ya Tanzanite One inayochimba madini ya Tanzanite, wilayani Simanjiro mkoani Manyara, imeanza ujenzi wa hospitali ya mama na mtoto, katika mji wa Mirerani ili kuwandolea  wananchi wa eneo hilo adha ya kutembea umbali mrefu kufuata matibabu.
Akizungumzia kuhusu ujenzi huo Mkurugenzi mwenza wa kampuni hiyo, Hussein Gonga amesema ujenzi wa hospitali hiyo, utagharimu zaidi ya Sh200 milioni .
Gonga amesema ujenzi wa hospitali hiyo ukikamilika  utawaondolea adha wananchi  hasa wanawake na watoto wanaoishi kwenye vijiji vilivyopo  maeneo  hayo kero ya kutembea umbali mrefu kufuata huduma za matibabu.
Amesema  kwa kushirikiana na wananchi na viongozi mbalimbali wa eneo hilo atahakikisha jengo hilo lina kamilika kwa wakati na kuanza kutoa huduma.
“Uamuzi wa kujenga jengo hili maalum ni moja ya mpango niliojiwekea mwaka huu ikiwamo kuokoa maisha ya mama na mtoto. Lakini pia  kuhakikisha jamii inayozunguka mgodi huu inaendelea kunufaika kwa uwepo wa kituo hiki,” amesema Gonga.
Mhandisi anayesimamia ujenzi  huo, Robert Mwanyika amesema ujenzi huo unatarajiwa kukamilika katika kipindi kisichozidi miezi mitatu.
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: