TLS kuhoji mahakamani uteuzi wa Jaji Mkuu


 1 Mei 2017



Rais wa TLS, Tundu Lissu 
Rais wa TLS, Tundu Lissu  
 Chama Cha Wanasheria Tanganyika (TLS), kimepanga kwenda mahakamani kupata ufafanuzi wa kisheria kuhusu nafasi ya Jaji Mkuu.
Rais wa TLS, Tundu Lissu alisema Baraza la Uongozi la chama hicho katika kikao chao kilichofanyika kwa siku mbili mjini Dodoma, wameamua kuwa na kauli moja ya kurudisha utawala wa sheria na hawawezi kukaa kimya wakati mambo yanakwenda ndivyo sivyo.
“TLS tumeamua kufungua mashauri Mahakama Kuu ya Tanzania kuhoji uhalali wa kikatiba wa Rais John Magufuli kushindwa hadi sasa kuteua kiongozi mkuu wa Mahakama ya Tanzania yaani Jaji Mkuu,” alisema Lissu.
Alisema kuwa baraza lao linaamini kuwa, Rais Magufuli anakiuka Katiba ya nchi ijapokuwa ana mamlaka kwa mujibu wa ibara ya 118 (4) inayomruhusu kuteua Jaji Mkuu iwapo itatokea nafasi hiyo kuwa wazi.
Alisema Kaimu Jaji Mkuu ni nafasi ya muda inayoshikiliwa na mtu mwenye sifa za kuwa Jaji Mkuu kabla haijajazwa na Jaji Mkuu kamili, lakini wanashangazwa na kauli aliyoitoa Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa Palamagamba Kabudi bungeni hivi karibuni kuwa mamlaka ya kukaimu hayana kikomo cha muda.
Pia, alisema wamepanga kuitisha mdahalo wa nchi nzima ambao utashirikisha viongozi wa Serikali, vyama vya siasa, wasomi, wanataaluma na waliokuwa wajumbe wa Tume ya Katiba ili kujua mustakabali wa suala hilo.

  Mshirikishe Mwenzako: zakacheka.blogspot.com/ www.zakacheka.simplesite.com +255 625966236





Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: