Upepo mkali kuvuma pwani ya Tanzania kesho


30 Mei 2017

Mtumbwi
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania imetoa tahadhari ya kuwepo kwa upepo mkali na mawimbi makubwa katika maeneo ya pwani ya Tanzania.
Maeneo yanayotarajiwa kuathirika ni mikoa ya Mtwara, Lindi, Pwani, Dar es Salaam, Tanga pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba.
Mamlaka hiyo, kupitia taarifa, imesema kunatarjiwa kuwepo na upepo mkali wa kasi ya kilomita 40 kwa saa na mawimbi yanayozidi mita 2.
"Msukumo wa upepo wa Kusi unatokana na kuimarika kwa mgandamizo mkubwa wa hewa katika ukanda wa pwani ya Tanzania," mamlaka hiyo ilisema.
"Watumiaji wa bahari na wakazi wa maeneo yaliyotajwa wanashauriwa kuchukua tahadhari na hatua stahiki."
Hali hiyo ya hewa inatarajiwa kuwepo hadi kufikia kesho 31 Mei.

Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: