Wanasayansi wagundua dawa ya magonjwa sugu


 30 Mei 2017


Aina mpya ya dawa hii ina nguvu mara elfu moja zaidi
Aina mpya ya dawa hii ina nguvu mara elfu moja zaidi
Wanasayansi nchini Marekani wamefanikiwa kupambana na maradhi yaliyokuwa sugu kwa dawa za kupambana na vijidudu yaani antibiotics tatizo ambalo lilikuwa tishio dhidi ya sekta ya afya duniani.
Watafiti wameiboresha dawa ya sasa, Vancomycin kwa kutengeneza aina nyingine ya dawa.
Vancomycin ilikuwa ikipoteza uwezo wake wa kupambana na bacteria aitwae enterococci ambaye husabisha madhara kwenye njia ya haja ndogo na vidonda.
Aina mpya ya dawa hii ina nguvu mara elfu moja zaidi na hushambulia vijidudu kwa njia tatu tofauti, kiasi cha vijidudu kushindwa kupambana na dawa hiyo.
Inakadiriwa kuwa vijidudu vilivyokuwa vikipambana na dawa za antibiotics husababisha vifo takriban elfu hamsini kila mwaka nchini Marekani na barani Ulaya.

Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: