Korea Kusini yataka mazungumzo na Korea Kaskazini


20 Julai 2017

Rais wa Korea Kusini Moon Jae in
Rais wa Korea Kusini Moon Jae in

Rais wa Korea Kaskazini Kim Jong un
Rais wa Korea Kaskazini Kim Jong un
Korea Kusini inasema kuwa imejiandaa kufanya mazungumzo ya kijeshi na jirani wake wa Korea Kaskazini , ijapokuwa Pyongyang bado haijatoa jibu lolote kuhusu wito huo ili kuanza mazungumzo mapema siku ya Ijumaa.
Uhariri wa gazeti kuu la Korea Kaskazini umesema ni upuzi mkubwa kwa Korea Kusini kupigania uhusiano mwema huku ikishikilia sera ya chuki dhidi ya Korea Kaskazini.
Rais wa Korea Kusini Moon Jae-in alipendekeza mazungumzo hayo ya ana kwa ana miaka mitatu iliopita ili kupunguza hali ya wasiwasi katika mpaka wa mataifa hayo.
Seoul pia imesema kuwa inatazama kwa karibu ishara zozote za uchokozi za Korea Kaskazini huku kukiwa na ripoti kwamba PyongYang ilikuwa inajiandaa kufanyia majaribio kombora jingine la masafa marefu.

Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: