Trump: Jeshi la Marekani liko tayari kuikabili Korea Kaskazini

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM

11 Agosti 2017

Zachary Bequeker  0625 966 236

Donald Trump na Mike Pence Bedminster, New Jersey, on 10 August 2017

Rais wa Marekani Donald Trump amesema jeshi la Marekani liko tayari kukabiliana na Korea Kaskazini wakati wowote ule.
"Suluhu ya kijeshi sasa ipo, imepangwa na iko tayari, Korea Kaskazini wakidhubutu kuchukua hatua isiyo ya busara. Twatumai Kim Jong-un atachagua njia nyingine!" Trump ameandika kwenye Twitter.
Amesema hayo huku Korea Kaskazini ikimtuhumu kwa kukaribia kutumbukiza rasi ya Korea katika vita vya nyuklia.
Pyongyang inakamilisha kuandaa mpango wake wa kurusha makombora karibu na kisiwa cha Marekani cha Guam.
Idara ya mambo ya nje katika kisiwa hicho katika bahari ya Pasifiki imetoa mwongozo Ijumaa pamoja na ushauri kwa wakazi wa kisiwa hicho kuhusu jinsi ya kujiandaa kukiwa na tishio la makombora.
Idara hiyo imewaonya raia wake wajiepushe kutazama mwanga kutoka kwa kombora kwani unaweza "kupofusha".
"Lala sakafuni na ukinge kichwa chako. Iwapo mlipuko utakuwa umbali kiasi kutoka ulipo, inaweza kuchukua sekunde 30 au zaidi kwa wimbi la mlipuko wenyewe kukufikia."
Bw Trump ameandika hivyo kwenye Twitter baada ya kutishia mapema wiki hii kupitia Twitter kwamba "Korea Kaskazini wasidhubutu kutoa vitisho zaidi kwa Marekani. Watajibiwa kwa moto na ghadhabu ambayo ulimwengu haujawahi kushuhudia."
Aidha, Ijumaa, shirika rasmi la habari la Korea Kaskazini KCNA liliituhumu Marekani kwa "jaribio la kihalifu la kusababisha mkasa wa kinyuklia katika taifa hilo la rasi ya Korea."
Shirika hilo lilisema Marekani inafanya kila juhudi kufanyia majaribio silaha zake za nyuklia katika rasi ya Korea.
Marekani ndiyo "mpanga njama ya tishio hili la nyuklia, mraibu wa vita vya nyuklia," taarifa ya KCNA imesema.
Awali, alikuwa ameitahadharisha Korea Kaskazini kwamba inafaa kuwa na "wasiwasi sana" iwapo itatenda lolote kwa Marekani.
Alisema utawala wa taifa hilo utakuwa shida kubwa "ambayo ni mataifa machache sana yaliyowahi kukumbana nayo" iwapo "hawatabadilika".
Kadhalika Bw Trump alikuwa awali ameshutumu serikali za awali za Marekani akisema zilionyesha udhaifu sana zikikabiliana na Korea Kaskazini na pia akashutumu mshirika wa karibu wa Korea Kaskazini, akisema kwamba inafaa "kufanya juhudi zaidi."
Alisema: "Nawaambia, iwapo Korea Kaskazini itafanya jambo lolote hata kwa kufikiria tu kuhusu kumshambulia mtu tunayempenda au tunayewakilisha au washirika wetu au sisi wenyewe inaweza kuwa na wasiwasi sana, sana."
"Nitawaambia ni kwa nini...ni kwa sabbau mambo yatawatendekea ambayo hawajawahi kufikirtia kwamba yanaweza kutokea."
Hata hivyo, aliongeza kwamba Marekani bado iko huru kushiriki katika mashauriano.
Aliongeza: "Nawaambia hivi, Korea Kaskazini inafaa kujiweka sawa au wataona shida kubwa kiasi ambacho ni nchi chache sana zilizowahi kushuhudia."
Haki miliki ya pich
Korea Kaskazini ilisema Jumatano kwamba inapanga kurusha makombora ya masafa wa wastani na ya masafa marefu kuelekea kisiwa cha Guam, ambapo kuna kambi ya ndege za kivita za kuangusha mabomu za Marekani.
Hata hivyo, kufikia sasa hakujakuwa na dalili zozote kwamba huenda kisiwa hicho cha Guam kikashambuliwa.

Kisiwa cha Guam na umuhimu wake

  • Kisiwa cha Guam kina ukubwa wa kilomita mraba 541 (maili mraba 209) na kinapatikana bahari ya Pasifiki kati ya Ufilipino na Hawaii.
  • Ni jimbo "lisilo na mpangilio wowote, na lisilojumuishwa kikamilifu" la Marekani, lenye wakazi karibu 163,000.
  • Kambi za jeshi la Marekani hutumia karibu robo ya ardhi ya kisiwa hicho. Marekani ina wanajeshi 6,000 kisiwa hicho na kuna mipango ya kuwasafirisha maelfu wengine huko.
  • Ni kituo muhimu katika shughuli za kijeshi za Marekani, ambapo huwezesha wanajeshi wa nchi hiyo kufika maeneo mengi muhimu Pasifiki, mfano eneo la bahari linalozozaniwa la South China Sea, rasi ya Korea na mlango wa bahari wa Taiwan.
Bw Trump alikuwa amewaambia wanahabari Jumanne kwamba: "Korea Kaskazini wasidhubutu kutoa vitisho zaidi kwa Marekani. Watajibiwa kwa moto na ghadhabu ambayo ulimwengu haujawahi kushuhudia."
Seneta mkongwe wa Marekani John McCain hata hivyo alikuwa na shaka kuhusu tamko la Trump.
"Viongozi wengi wakuu ambao nimewahi kuwaona, huwa hawatoi vitisho ikiwa hawako tayari kuvitekeleza na sina uhakika kwamba Rais Trump yuko tayari kuchukua hatua," alisema Bw McCain.
Korea Kaskazini ilikuwa imeghadhabishwa na vikwazo vipya ilivyowekewa na Umoja wa Mataifa siku ya Jumamosi.
Vikwazo hivyo vina lengo la kupunguza mapato kutoka kwa mauzo ya bidhaa nje ya Korea Kaskazini kwa theluthi moja.
KCNA imesema Korea Kaskazini, ambayo imefanyia majaribio silaha za nyuklia mara tano, itajibu vikali na kwamba "Marekani italipia" kwa kuchangia kutunga vikwazo hivyo.
Waziri mkuu wa Australia Malcolm Turnbull amesema taifa lake liko tayari kushiriki katika vita dhidi ya Korea Kaskazini iwapo nchi hiyo ya rasi ya Korea itatekeleza shambulio dhidi ya Marekani.
"Iwapo kutakuwa na shambulio dhidi ya Marekani, Mkataba wa Anzus wa mwaka 1951 utaanza kutekelezwa na Australia itajitokeza kuisaidia Marekani," alisema kwenye mahojiano na kituo kimoja cha redio, "vile vile ambavyo Marekani ingefika kutusaidia iwapo tutashambuliwa."
Nijuze habari kwa 0625 966 236
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: