IBADA YA KUMWOMBEA LISSU

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM

10 Sep 2017

Mdogo wake Tundu Lissu, Vicent Lissu akiwa na
Mdogo wake Tundu Lissu, Vicent Lissu akiwa na Mbunge wa Ubungo Saed Kubenea walipohudhuria Ibada katika kanisa la ufufuo na Uzima.
Vincent, mdogo wake Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu amesema kabla ya kaka yake kushambuliwa kwa kupigwa risasi aliwaeleza kwamba kuna mtu anafuatilia gari lake.
Akizungumza wakati wa ibada ya kumwombea Lissu iliyofanyika katika Kanisa la Ufufuo na Uzima leo Jumapili, amesema alimwona kaka yake akiwa amelala kitandani hospitalini mwili ukiwa na damu.
Amesema alipoamka leo asubuhi alielezwa na mtu kuwa kuna ibada maalumu ya kumwombea Lissu, hivyo akaamua kuhudhuria katika kanisa hilo la Mchungaji Josephat Gwajima.
Vincent amesema baada ya kaka yake kushambuliwa Alhamisi wiki hii, alienda Dodoma na kwamba anawashukuru madaktari waliofanya kila waliloweza kuokoa maisha ya ndugu yake.
Amesema kaka yake ni mpenda haki tangu akiwa mdogo na ameomba wananchi wazidi kumuombea.
Lissu hivi sasa anaendelea na matibabu katika Hospitali ya Aga Khan jijini Nairobi nchini Kenya.
Katika shambulio lililofanywa na watu wasiofahamika nyumbani kwa Lissu Area D mjini Dodoma, mbunge huyo alipigwa risasi tano.
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: