RAIS WA UFARANSA ATAKA KUWEPO JESHI LA MUUNGANO WA ULAYA

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM
26 Sep 2017French President Emmanuel Macron delivers a speech on the European Union at the Sorbonne University on 26 September 2017 in Paris
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron
Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, ametoa wito wa kutaka kubuniwa kikosi cha pamoja cha jeshi kama sehemu ya maono yake ya siku za usoni kwa muungano huo.
Bwana Macron alipendekeza kuwa kikosi hicho kipya kitakuwa ni sehemu ya Nato.
Aliingia madarakani mwezi akiahidi kuchangia udhabiti Ulaya.
Wakati wa hotuba kuu kwenye chuo cha Sorbonne mjini Paris, Bw Macron alisema anataka muungano wa Ulaya kuboresha mifumo yake ya ulinzi kwa kubuni jeshi la pamoja.
Hakutoa taarifa zaidi lakini alisema kuwa kikosi hicho kitakuwa sehemu ya Nato na kinatajiwa kuanza huduma ifikapo mwaka 2020.
Nchi kadha za Muungano wa ulaya sawa na kamishina wa tume ya Ulaya Jean-Claude Juncker, awali wamesema kuwa kunastahili kuwepo jeshi la pamoja na Ulaya kukabiliana na Urusi na vitisho vingine.
Lakini Uingereza imeonya kuwa hatua hiyo itahujumu kikosi cha Nato
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: