NEW ZEALAND KUONGOZWA NA WAZIRI MKUU MWANAMKE

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM
19 0ktoba 2017
Jacinda Ardern
New Zealand inajiandaa kwa serikali ya Muungano ambayo itaongozwa na kiongozi wa chama cha Labour, Jacinda Ardern
Bi Ardern amekuwa kiongozi wa upinzani kwa miezi mitatu sasa. Katika umri wa miaka 37 anataraji kuwa waziri mkuu mwenye umri mdogo zaidi nchini New Zealand tangu mwaka 1856.
Chama chake cha Lebour kilichukua nafasi ya pili mwezi Septemba ambapo hakuna chama kiliweza kupata wingi wa kura.
Sasa kinatarajiwa kuingia madarakani baada ya chama kidogo cha New Zealand First party kukubali kujiunga na serikali.
Muungano huo mpya pia utaungwa mkono na chama cha Green Party.
Jacinda Ardern with political supporters


Haki miliki ya pich

Jacinda Arden tayari ameonyesha kuwa anaweza kufanya kampeno nzuri na kufanya mikataba ya kisiasa lakini bado anakabiliwa na chamgamoto mpya.
Kwanza ni kuwashawishi watu nchini New Zealand ambao hawakumpigia kura kuwa chama hicho ambacho kilichukua nafasi ya pili kitaongoza.
Pia kuna uhusiano wa kujengwa na serikali ya Australia ambayo ilikilaumu chama cha New Zealand Labour party kwa upinzani dhidi yao wakati wa suala ya uraia mara mbili.
FACEBOOK: zakacheka.blogspot.com na download App ya ZAKACHEKA huko
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: