Mwanajeshi mmoja wa Korea Kaskazini amepigwa risasi na kujeruhiwa na wanajeshi wenzake akijaribu kuvuka kwenda Korea Kusini

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM

Mwanajeshi mmoja wa Korea Kaskazini amepigwa risasi na kujeruhiwa na wanajeshi wenzake wakati akijaribu kuvuka kwenda Korea Kusini akipitia mpaka wenye ulinzi mali.
Hata hivyo mwanajeshi huyo alifanikiwa kuvuka mpaka na sasa anaendelea kupata nafuu.
Alipigwa risasi kwenye mkono wake na pia kwenye bega.
Mwanajeshi huyo alivukia katika kijiji cha Panmunjon, ambapo makubaliano ya kumaliza vita vya Korea yalisainiwa mwaka 1953.
Karibu watu 30,000 raia wa Korea Kaskazini wamehamia Korea Kusini tangu wakati huo lakini wengi huvuka kupitia China
Si jambo la kawaida kwa mtu yeyote kuvuka mpaka unaotenganisha nchi hizo mbili.
Hiki ndicho kisa cha nne cha mwanajeshi wa Korea Kaskazini kuvuka kupitia eneo lenye ulinzi mkali.
Korea Kaskazini na Kusini wako kwenye mzozo mkubwa tangu vimalizike vita mwaka 1953 na hakuna makubaliano rasmi ya amani yaliyotiwa sahihi kati yao.

Tuma habari picha WhatsApp 0625966236

Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: