Rais mstafu wa CWT ashikiriwa na TAKUKURU

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM=>
Hutyyyhgg

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa TAKUKURU inamshikilia Rais mstaafu wa Chama Cha walimu Tanzania (CWT) Gracian Mkoba kwa tuhuma za rushwa.

Hilo limethibitishwa na Afisa Uhusiano wa TAKUKURU Makao Makuu, Mussa Misalaba, ambaye amesema wanamshikilia Mkoba kwa tuhuma za kugawa fedha kwa baadhi ya wajumbe wa mkutano mkuu wa chama hicho ili kuwashawishi wamchague mgombea anayemtaka.

"Mukoba ameshastaafu, lakini kuna mgombea mmoja alikuwa anataka achaguliwe, tumemkamata leo asubuhi akigawa rushwa kuwashawishi wapiga kura kwenye ukumbi wa Chimwaga wamchague huyo mgombea wake," amesema Misalaba.

Misalaba ameongeza kuwa TAKUKURU inaendelea kufanya uchunguzi zaidi dhidi ya Mukoba kabla ya kumfikisha mahakamani.

Mukoba anakuwa mtu wa tatu kukamatwa na TAKUKURU kwa tuhuma za rushwa kwenye uchaguzi ndani ya wiki moja, wengine ni aliyekuwa Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM), Sadifa Juma Khamis na mfanyabiashara Haider Gulamali.
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: