Mawaziri wawili wa zamani wakamatwa kwa tuhuma za rushwa Zimbabwe

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM=>

Mawaziri wawili wa zamani wa Zimbabwe wamefikishwa mahakamani kwa tuhuma za rushwa.
Samuel Undenge ambaye alikua waziri wa nishati anatuhumiwa kutumia dola elfu kumi na mbili kwa kampuni ambayo haukufanya lolote.
Kwa upande wa wake Walter Mzembi aliyekuwa waziri wa mambo ya nje wakati wa utawala wa Robert Mugabe aliyeondolewa madarakani mwezi Novemba, anatuhumiwa kuchangia baadhi ya mali za televisheni ya Taifa kwa kanisa moja nchini humo bila ya idhini ya serikali.
Wote wawili wamekana mashitaka hayo.Inatarajiwa kesi hizo zitasikilizwa tena baadae mwezi huu.
Rais mpya Emmerson Mnangagwa ameapa kupambana na rushwa iliyodumu karibia wakati wote wa utawala wa Robert Mugabe.
•Wasiliana nasi kwa +255625966236
Pia tembelea blog hii kwa neno la Mungu :-
www.zakachekainjili.blogspot.com
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: