Polisi wamshikilia Muisrael anayeuza viungo vya binaadam Cyprus

ZAKACHEKA.BLOGSPOT.COM=>
Polisi nchini Cyprus wanasema wanamshikilia raia mmoja wa Israel anayetuhumiwa kufanya biashara ya viungo vya binadam.
Moshe Harel amehusishwa kufanya biashara ya figo kwa matariji wa Israel takriban miaka kumi sasa.
Amehusishwa kuchukua figo za raia wa Kosovo pamoja na Uturuki na nchi nyingine kadhaa ambao mpaka sasa hajawalipa chochote.
Msemaji wa polisi nchini Cyprus amesema mtu huyo alikamatwa uwanja wa ndege wa Larnaca mwezi Desemba.
Anatarajiwa kufikishwa mahakamani siku ya Jumanne kujibu mashtaka yanayomkabili.
Anahitajika kwa makosa kama hayo nchini Kosovo.
*Wasiliana nasi kwa +255625966236*
Pia tembelea blog yetu kwa neno la Mungu:-
www.zakachekainjili.blogspot.com
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: