Baba amrusha mwanaye wa mwaka mmoja kutoka juu ya paa

Mwanaume mmoja kutoka nchini Afrika Kusini ameingia kwenye headlines za vyombo vya habari duniani kwa kitendo alichokifanya cha kushangaza baada ya kumtupa mtoto wake kutoka juu ya bati la nyumba yake.

Inaelezwa kuwa mwanaume huyo ambaye ana umri wa miaka 38 nyumba yake ilitakiwa kubomolewa na polisi kutokana na kuishi katika makazi ‘haramu’ na katika kufanyika kwa zoezi hilo aliamua kupinga nyumba yake kubomolewa kwa kutishia kumtupa mtoto wake.
Mwanaume huyo alipanda juu ya nyumba yake akiwa amemshikilia mtoto wake huyo wa kike wa mwaka mmoja na pindi askari alipomsogelea alimwachia mtoto huyo na bahati nzuri alidakwa na moja ya maaskari waliokuwa eneo hilo.

Mtoto huyo anaripotiwa kutojeruhiwa na mwanaume huyo amekamatwa na kufunguliwa kesi ya jaribia la kuua.

Download App Yetu hapa chini, Bonyeza picha:-



Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: