Mtoto azaliwa miaka 4 baada ya wazazi wake kufariki

Mtoto amezaliwa China kupitia mwanamke aliyebeba uja uzito, miaka minne baada ya wazazi wa mtoto kufariki ktaika ajali ya gari, vyombo vya habari China vinaripoti.
Wazazi hao waliofariki mnamo 2013, walitoa mayai kadhaa yaliogandishwa kwa matumaini kwamba watazaa kupitia mfumo wa IVF.
Baada ya ajali wazazi wao waliwasislisha kesi kuruhusiwa kuyatumia mayai hayo.
Mtoto huyo mchanga wa kiume alizaliwa Desemba kupitia mwanamke aliyebeba mimba huko Laos na kisa hicho kiliripotiwa kwa mara ya kwanza wiki hii na gazeti la The Beijing News.
Gazeti hilo limeeleza jinsi hakujawahi kushuhudiwa kesi ya aina hiyo na ndio sababu iliyowalazimu wazee wa wazazi wa mtoto huyo kuwasilisha kesi kabla ya kuanza mpango wa kutafuta mbebaji mimba hiyo.

Kisa cha kwanza cha aina yake

Wakati wa ajali hiyo, mayai yalikuwa yamehifadhiwa vizuri katika hospitali huko Nanjing na yalikuwa yamegandishwa katika nyuzi joto ya chini ya 196 katika tanki lililojaa gesi lya maji ya NItrojini.
Kesi hiyo mahakamani iliwaruhusu bibi na babu wa mtto huyo kumiliki mayai hayo yaliogandishwa.
Hakukuwepo kesi ya aina hiyo awali kuweza kusaidia kujua iwapo wanaweza kurithi mayai ya watoto wao , kwa mujibu wa ripoti.
Wodi ya watoto ChinaHaki miliki ya pichaCHINA PHOTOS
Image captionBibi na Babu ya mtoto huyo wanasema wamefurahi sana kwamba kizazi chao sasa kitaendelea (picha ya zamani)
Hatimaye waliruhusiwa kuyatumia mayai hayo, lakini tatizo jingine likazuka. Mayai hayo yangeweza kutolewa katika hospitali ya Nanjing iwapo tu kungekuwa na ithibati kuwa hospitali nyingine iko tayari kuyahifadhi.
lakini kutokanana wasiwasi wa kisheria kuhusu mayai ambayao hayajapandikizwa, ilikuwa ni vigumu kupata taasisi nyingine ya afya China iliyotaka kujihusisha.
Na kutokana na kwamba ubebaji mimba ya mtu mwingine ni haramu China, nafasi iliyosaliua ilikuwa ni kutafuta mbebaji mimba katika nchi ya nje.

Kuthibitisha uzazi na uraia

Hatimaye, babu na bibi yake mtoto huyo walishirikiana na shirika linalotafuta wanawake wanaobeba mimba za watu wengine na waliangukia eneo la Laos, ambako mpango huo unaruhusiwa kisheria.
Kwasababu hakuna ndege inayobeba gesi ya nitrojini kiwango cha kujaa chupa ya chai, mzigo huo adimu ulisafirishwa kwa gari.
Kijiji ambacho wanaume wengi ni makapera China
Na huko Laos, mayai yalipandikizwa ndani ya kizazi cha mama mbebaji na ilipofika Desemba 2017 mtoto huyo wa kivulana alizaliwa.
Uraia wa mtoto huyo, aliyepewa jina Tiantian, lilikuwa ni tatizo jingine na kwahivyo waliamua azaliwe China na sio Laos - ambapo ilibidi mwanamke huyo asafirishwe kwa viza ya kitalii.
Download App Yetu hapa chini, Bonyeza picha:-



Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: