Waziri Mpango apangua Hoja za CAG kuhusu Deni la Taifa

Waziri wa Fedha na Mipango, Dk Phillip Mpango amesema Tanzania inao uwezo wa kukopa ndani na nje ya nchi kutokana na viashiria vilivyopo.

Waziri Mpango ameyasema hayo leo Aprili 12 katika mkutano na wanahabari alipokuwa akijibu baadhi ya hoja zilizopo kwenye ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) ya mwaka wa fedha ulioishia Juni 30, 2017 mjini Dodoma.

“Tunapofanya tathmini ya uhimilivu wa deni la taifa, uwiano tunaouangalia siyo deni la taifa kwa pato la taifa peke yake, tunaangalia vigezo vingi,” amesema.

Amesema taifa lina uwezo wa kuendelea kukopa na si kwa kuangalia uwiano wa deni na pato la taifa peke yake.

“Takwimu nilizonazo ni za sasa, ile ripoti ya CAG ilikuwa inaishia 2017. Nitawapa taarifa za sasa,” amesema Dk Mpango na kuongeza:

 “Tulifanya tathmini ya uhimilivu wa deni Novemba 2017. Thamani ya sasa ya jumla ya deni la taifa kwa pato la taifa ni asilimia 34.4, ukomo wake kimataifa ni asilimia 56 kwa hiyo hapo tupo vizuri.”

Download App YETU hapa⬇⬇



Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: