Aomba msamaha kwa picha ya 'kichwa cha Trump kilichokatwa'


31 Mei 2017

Kathy Griffin amekuwa mkosoaji mkubwa wa utawala wa Trump
Kathy Griffin amekuwa mkosoaji mkubwa wa utawala wa Trump
Mcheshi mmoja nchini Marekani ameomba msamaha kuhusu picha ambayo alionekana amebeba kichwa kilichokatwa kinachofanana na na ra Donald Trump .
Katika ujumbe wa kanda ya video iliochapishwa katika mtandao wa Twitter Kathy Griffin aliomba kusamehewa na kusema kuwa alikuwa amepita mpaka.
Alisema kuwa alimuomba mpiga picha wa watu maarufu Tyler Shield kuondoa picha hiyo katika mtandao.
Picha hiyo ya kutisha ilizua pingamizi katika mitandao ya kijamii ikiwemo kutoka kwa mwana wa Trump Donald Trump Jr.
''Inatatiza lakini sio ajabu'' ,alituma ujumbe katika mtandao wa Twitter, ''hivi ndivyo ubaya wa siku hizi, wanachukulia hili kuwa sawa''.
Mwana wa aliyekuwa mpinzani wa Trump katika uchaguzi wa Marekani Hillary Clinton, Chelsea alishutumu picha hiyo akisema kuwa inaonyesha unyonge na makosa.
''Sio vizuri kufanyia mzaha wa kumuua rais'', alituma ujumbe katika mtandao wa Twitter.
Aliyekuwa mgombea wa tiketi ya urais wa chama cha Republican Mitt Romney pia naye alituma ujumbe katika mtandao wa Twitter akisema: Siasa zetu zimekosa mwelekeo lakini chapisho hilo la Kathy Griffins linaonyesha uchafu uliopo na makosa makubwa tunayofanya.
Mshindi huyo wa tuzo la uigizaji la Emmy na mcheshi amekuwa mkosoaji mkubwa wa utawala wa Trump.
Katika kanda ya video akiomba msamaha ,alisema: Sasa naona ukweli wa picha hizo.Mimi ni mcheshi lakini nilipita mipaka. Picha hizo zinakera.Ninaelewa vile zinavyowaathiri raia.Hazina tena ucheshi.naomba msamaha.
   Bonyeza hapa kwa habari zingine: zakacheka.blogspot.com  +255 625966236


Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: