Juventus yatinga fainali


10 Mei 2017
Wachezaji wa klabu ya Itali Juventus wakisheherekea ushindi wao dhidi ya Monaco
Haki miliki ya picha
Klabu ya Juventus kwa mara ya pili imefuzu katika fainali ya kombe la vilabu bingwa Ulaya baada ya kuishinda Monaco kwa jumla ya mabao.
Wakiwa wanaongoza 2-0 katika awamu ya kwanza ya mechi ,timu hiyo ya Itali iliongeza jumla ya mabao wakati mshambuliaji wao Mario Mandzukic alipofunga .
Dani Alvez aliongeza bao la pili baada ya kipa Danijel Sabusics kuupangua mpira ulioanguka mbele yake.
Kylie Mbappe alifunga krosi iliopigwa katika kimo cha nyoka ya Joao Moutinho ili kufunga bao la kufutia machozi, lakini klabu hiyo ya ligi ya daraja la kwanza haikuweza kufunga zaidi ya bao moja.
Juventus ambao hawajashinda kombe hilo tangu 1996 na waliopoteza katika fainali ya mwaka 2015 dhidi ya Barcelona watakabiliana na Real Madrid au Atletico Madrid katika uwanja wa Cardiff mnamo tarehe 3 mwezi Juni.
Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: