Mwanamume aliyewachoma kisu wageni Zanzibar asakwa


31 Mei 2017

Visiwa vya Zanzibar hutegemea sana utalii
Visiwa vya Zanzibar hutegemea sana utalii
Polisi visiwani Zanzibar wanamsaka mwanamume mmoja anayedaiwa kuwachoma kwa kisu watu sita wakiwemo raia wanne wa kigeni na kuwajeruhi vibaya usiku wa kuamkia Jumatatu.
Mwanamume huyo aliwashambulia wageni hao katika mgahawa wa Lukman Mkunazi Mjini Zanzibar.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja, Hassan Nassir Ali aliwaambia waandishi wa habari Jumatatu kuwa mtuhumiwa aliyetenda hayo hayatambuliwa kwa jina.
Hata hivyo, anafahamika kwa sura na, anakisiwa kuwa na umri wa miaka 25.
Bw Ali alisema uchunguzi wa awali umebaini mtuhumiwa huyo alifika katika mgahawa huo na kuwachoma watu watatu ambao walikuwa mgahawani hapo kwa ajili ya kujipatia chakula na kisha akakimbia na akiwa njiani akawashambulia wengine watatu.
Walioshambuliwa ni Mauget Gerarol ambaye ni raia wa Ufaransa, Liying Liang raia wa Canada na Jennifer Wolf na Anna Catharina ambao ni raia wa Ujerumani.
Wengine ni Hassan Abdallah na Sajad Hussein.
Kwa mujibu wa gazeti la Mwananchi, Bw Ali alisema majeruhi wote walipatiwa matibabu na kuruhusiwa lakini Mauget Gerarol raia wa Ufaransa bado amelazwa hospitalini.
Zanzibar hutegemea sana utalii.

Share on Google Plus

ABOUT BLOGGER INJILI HALISI MINISTRY

Hi! I am Zachary John Bequeker, from Mwanza Tanzania, East Africa.I'm a blogger of ZAKACHEKA NEWS LINE And ZAKKACHEKA INJILI.Contact me +255 625966236 / +255 758590489 or mail on zacharybequeker@gmail.com . Thanks!!!

0 Post a Comment: